MAANA YA CHAMA CHA WAFANYAKAZI
Chama cha wafanyakazi ni Chama cha hiari na kidemokrasia ambacho kinaundwa na wafanyakazi kwa madhumuni ya kulinda na kudumisha maslahi yao ya pamoja na kuboresha hali zao za maisha.
Kifungu cha Nne (4) cha sharia ya Ajira na mahusiano Kazini, 2014 kuhusu tafsiri kinaeleza kwamba “Chama cha Wafanyakazi’’ maana yake ni idadi yoyote ya wafanyakazi walioungana pamoja kwa lengo, ikiwa kwa lengo hilo tu au kwa malengo mengine, la kuratibu mahusiano kati ya wafanyakazi na waajiriwa wao au Chama cha waajiri ambako waajiri wamejiunga.
Kazi (Functions) za Chama cha wafanyakazi ( Trade union Representatives) zimeainishwa katiak Kifungu cha 62(40 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini, 2004.
KAZI ZA VIONGOZI WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI MAHALI PA KAZI
Viongozi wa chama cha wafanyakazi kwa ujumla wao hufanya kazi ambazo ni za Chama cha wafanyakazi kw mujibu wa Katiba ya Chama ama kwa mujibu wa Sheria. Katika kulinda na kudumisha maslahi ya wafanyakazi na kufikia malengo yake Chama cha Wafayakazi kupitia niongozi wake hufanya kazi nyingi mahali pa kazi katika ngazi mbalimballi kam ifuatavyo;
Vile vile viongozi wanatakiwa kuwawakilisha wafanyakazi katika shughulikia masuala mbalimbali katika vyombo vifuatavyo.
WAJIBU/MAJUKUMU YA VIONGOZI WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI
Kama vile kiongozi wa chama cha wafanyakazi alivyo na haki zake, pia kwa upande mwingine ana wajibu au majukumu yanayokwenda sambamba na haki hizo. Yafuatayo ni daadhi ya majukumu yake;